
Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla
RC Makalla amesema hayo wakati wa kikao kazi kati yake na wakurugenzi wa Halmashauri na TARURA kilicholenga kuondoa kero ya tozo ya 'wrong parking'.
Aidha, RC Makalla amesema kikao hicho wamekubaliana tozo ya 'wrong parking' itekelezwe kwa mujibu wa sheria na kwa ambaye ataonekana alidhamiria moja kwa moja kuvunja sheria huku akisisitiza elimu iendelee kutolewa.