Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Malavane, Maputo, Rais Dkt. Mwinyi amepokelewa na viongozi mbalimbali wa nchi hiyo pamoja na gwaride rasmi lililoandaliwa kwa ajili yake.
Mkutano huo wa siku moja unawahusisha wakuu wa nchi wanachama wa SADC na miongoni mwa mambo yatakayojadiliwa ni masuala ya usalama na hatua za kukabiliana na vitendo vya ugaidi katika nchi wanachama wa jumuiya hiyo.