
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa
Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa Polisi mkoani humo Simon Maigwa, wakati wa ukaguzi wa mabasi yanayofanya safari za masafa marefu kutoka katika kituo kikuu cha mabasi cha Moshi mkoani humo.
Ambapo katika ukaguzi huo baadhi ya mabasi yamebainika kuwa na hitilafu katika mifumo ya breki na injini na kusababisha kuzuiwa kuendelea na safari hadi pale yatakapofanyiwa matengenezo na kukaguliwa upya.