Kushoto ni Grayson Mahembe Askari aliyejinyonga, na kulia ni Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mtwara ACP Mark Njera
Askari huyo alijinyonga Januari 22 mwaka huu kwa kutumia tambala la kudekia akiwa mahabusu ya kituo cha polisi wilaya ya Mtwara.
Katika taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Mtwara ACP Mark Njera, alikiri kuwa askari wake saba wanaotuhumiwa kutekeleza mauaji ya kijana Mussa Hamisi (25), mkazi wa kijiji cha Ruponda wilaya ya Nachingwea mkoani humo aliyekuwa akiwadai askari hao zaidi ya shilingi milioni 33.7 wameshafikishwa mahakamani
Imeelezwa kuwa tukio la mauaji ya kijana huyo walilitekeleza Januari 5, 2022 na mwili wa marehemu waliutupa katika kitongoji cha Majengo, kijiji cha Hiari wilayani Mtwara.