Jumatatu , 11th Jul , 2022

Raila Odinga (77) kwa sasa yupo kwenye jaribio lake la nne la kuwania Urais wa Kenya katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe  9  mwezi ujao, ana historia ya kukaribia kuutwaa uongozi huo wa juu wa nchi kwenye uchaguzi wa 2008 wakati alipoukosa na kuteuliwa kuwa Waziri Mkuu.

Raila Odinga, Mgombea Urais nchini Kenya

Baba yake aliwahi kuwa Naibu Rais wa Kenya baada ya uhuru, Raila amekua akijulikana kwa majina kadhaa na wafuasi wake huku jina maarufu akiitwa Baba. Majina mengine ni "Agwambo" (ikitafsiri Matendo ya Mungu) pamoja na Tingatinga (jina allilowahi kuitwa hayati Rais Dkt. John Magufuli).