
Noti Mpya Zimbabwe
Taifa hilo linalokabiliwa na ukata linatarajia kutambulisha noti zake hizo ambazo zimepingwa mno na watu, na kuibua kumbukumbu mbaya ya mwaka 2009 wakati watu waliposhindwa kuweka akiba benki kutokana na mfumuko wa bei wa asilimia milioni 231.
Maelfu ya watu nchini Zimbabwe wamekuwa wakilala nje mashine za kutolea fedha za mabenki (ATM) wakingojea kutoa fedha zao, wengi wao ikiwa ni za dola ya Marekani ambayo imekuwa ikitumika kwa sasa nchini humo.