Mama mzazi wa mtoto huyo Upendo Lendoya amesema mtoto wake ameuawa na wifi yake na hana la kufanya anatafakari kilichotokea.
Wakazi wa kijiji hicho wamegoma chakula kupikwa kwenye msiba huo kutokana na mauwaji ya kikatili yaliyofanyika kwa mototo huyo na kutokuwa na ushirikiano wa ndugu wa marehemu
Naye Kamanda wa Polisi mkoa wa Manyara George Katabazi amesema uchunguzi bado unaendelea na pindi utakapo kamilika mtuhumiwa atapewa haki yake huku mwakilishi wa dawati la jinsia akihamasisha Amani itawale kwenye kijiji hicho hadi upelelezi ukamilike