
"Mtu anayekiuka masharti ya kifungu hiki anatenda kosa na, akitiwa hatiani, atawajibika kulipa faini isiyozidi Ksh100,000 za Kenya au kifungo kisichozidi miezi mitatu au vyote kwa pamoja," yanaelezea maandishi ya mswada huo.
Mswada huo pia unampa Katibu wa Baraza la Mawaziri mamlaka ya kuteua maeneo ya maandamano baada ya mashauriano na serikali za kaunti. Hii itajumuisha maeneo ya kuagiza ambapo maandamano ya umma yanaruhusiwa, pamoja na maeneo ambayo yamepigwa marufuku.
Mswada huo pia unampa Katibu wa Baraza la Mawaziri mamlaka ya kuteua maeneo ya maandamano baada ya mashauriano na serikali za kaunti. Hii itajumuisha maeneo ya kuagiza ambapo maandamano ya umma yanaruhusiwa, pamoja na maeneo ambayo yamepigwa marufuku.
Ikumbukwe kuwa Muswada wa sheria ya marekebisho ya mfumo wa umma wa 2025 ulipendekeza mabadiliko ya Sheria iliyopo ya Mfumo wa Umma (Sura ya 56) kwa kuweka vikwazo vya mikusanyiko kwenye maeneo ya mikutano ya hadhara.
Mapendekezo ya Passaris yameibua gumzo kwenye mitandao ya kijamii, huku baadhi wakiupinga.
Muswada huu wa Mbunge Passaris unakuja huku maandamano ya vijana wanaofahamika kama Gen Z yakipangwa kufanyika tena tarehe 7 July, kupinga muswada wa fedha 2025.