
Patrick Mususa
Meneja Miradi na Uendelezaji Biashara wa soko hilo Patrick Mususa amesema katika kipindi hicho, idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa imeongezeka mara mbili kutoka hisa 869,453 hadi hisa milioni moja na laki nane.
Mususa ameongeza kuwa ukubwa wa mtaji wa soko umepanda kwa asilimia 0.4 huku ukubwa wa mtaji wa makampuni ya ndani pia ukiwa umepanda kwa asilimia 0.3 na kufikia shilingi trilioni 8.21 kutoka shilingi trilioni 8.19.