Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora, Emmanuel Nley.
utakapokamilika atafikishwa mahakamani.
Akizungumza na www.eatv.tv, Kamanda Nley amesema kuwa uchunguzi huo ukikamilika mtuhumiwa atapandishwa kizimbani kujibu tuhuma zinazomkabili.
"Sisi kazi yetu kukamilisha uchunguzi tu, utakaohusisha mashuhuda pamoja na majirani wa eneo husika na baada ya hapo faili litakabidhiwa sehemu husika, kazi yetu itakuwa imeishia hapo", amesema Kamanda Nley.
Tukio hilo litokea, Januari 27, 2019 saa moja usiku katika eneo la Kariakoo mjini humo, ambapo mtuhumiwa alimvizia mwanajeshi huyo akiwa nyumbani kwake na kumkaba shingoni kisha kumuangusha chini na katika purukushani za kutaka kumbaka huku akimkaba shingoni alisababisha kifo chake.





