Jumatano , 23rd Nov , 2022

Kijana mdogo ameuawa na watu wengine 14 wamejeruhiwa katika mashambulizi mawili yanayoshukiwa kuwa ya mabomu katika vituo vya mabasi mjini Jerusalem.

Polisi mjini humo wamethibitisha Milipuko hiyo iliyotokea katika maeneo mawili yenye shughuli nyingi nje kidogo ya mji wakati watu walipokuwa wakielekea kazini.

Mvulana aliyefariki ni miongoni mwa watu 12 waliojeruhiwa na mlipuko wa kwanza. Wengine watatu walijeruhiwa na mlipuko wa  pili.

Waziri wa usalama wa ndani wa Israel alisema katika eneo moja kwamba hili ni "shambulio ambalo hatujatokea kwa muda mrefu".

Mwaka huu umeshuhudia wimbi la mashambulizi mabaya ya bunduki na kisu yakiwalenga Waisraeli, na kusababisha mawimbi ya uvamizi wa jeshi la Israel katika miji ya Palestina katika Ukingo wa Magharibi. Lakini matumizi ya vilipuzi mjini Jerusalem yatakuwa mashambulizi makubwa zaidi ya aina yake katika miaka mingi.