Mkaguzi na mdhibiti mkuu wa serikali nchini Tanzania CAG Ludovick Utouh.
Ripoti ya CAG ya ukaguzi wa mashirika ya Umma kwa mwaka 2013/2014 iliyowasilishwa Bungeni mjini Dodoma imesema mapendekezo hayo yaliwasilishwa kwa mara ya kwanza 2008/2009.
Aidha CAG alisema kanuni za utawala bora zinahitaji watendaji wakuu wa mashirika ya Umma wateuliwa na bodi ya wakurugenzi wa mashirika hayo badala ya kazi hiyo kufanywa na Rais.
