Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kubenea amtolea uvivu Sakaya

Ijumaa , 14th Jul , 2017

Kaimu Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani CHADEMA , Saed Kubenea amemtolea uvivu mbunge wa jimbo la Kaliua Magdalena Sakaya kwa kudai CHADEMA haijaingilia ugomvi wa chama chao bali wanataka kumaliza mgogoro uliopo kwa kuwaondoa mamluki.

Akizungumza na Wanahabari Mh. Kubenea amesema kwamba CHADEMA imeamua kujitosa katika mgogoro wao baada ya kuombwa na wabunge wa chama hiko wakiongozwa na viongozi waandamizi akiwepo Maalim Seif Sharif Hamad.

"Sakaya ananituhumu  na kusema CHADEMA tunawaingilia CUF, nataka niseme kwamba hatujaingilia ugomvi wao, pili Sakaya siyo mwanachama wa CUF kwani alikwisha vuliwa uanachama na akafukuzwa, pia hana uongozi wowote ndani ya chama hicho kwani hata barua yake ya rufaa mpaka leo haijakubalika, na Naibu Katibu Mkuu mimi ninayemtambua ni Bashange na siyo yeye" Kubenea.

Aidha Kubenea ameongeza kuwa

"Matukio yote ambayo CUF wamekuwa wakitendeana  kama Lipumba na genge lake kuvamia mkutano CHADEMA hatukuwepo, sasa kwa vile wameomba msaada kwetu sisi tumeanzisha oparesheni ondoa msaliti Buguruni ambayo tutaifanya kwa ukamilifu. Tumeagizwa na kamati kuu kuikomboa CUF", aliongeza Kubenea.

Pamoja na hayo Kubenea amesema lengo la CHADEMA kumsaidia Maalim Seif vita yake na Prof. Lipumba ni kuinusuru chama chao kilichopo ndani ya mwamvuli wa UKAWA kisije kikaingia kwenye migogoro inayosababishwa na CCM ili kuua upinzani ndani ya Tanzania.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala