
Picha ikionesha mkono uliojeruhiwa na Mbwa.
Akizungumza na EATV jijini Dar es Salaam wakati wa mahojiano, mtaalamu wa afya ya jamii kutoka Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto, Jubilate Bernard amesema wapo watu katika jamii wanahusisha dalili za ugonjwa huo na mambo ya kishirikina kitu ambacho sio sahihi.
Jubilate amesema kuwa, “Siku ya kichaa cha mbwa huadhimishwa kila Septemba 28, duniani ambapo jumuiya ya kitaifa inatoa elimu juu ya ugonjwa huo kwa duniani nchi ya India inaongoza kuwa na ugonjwa na kufuata bara la Afrika.
“Watu 5,9000 hupoteza maisha kutokana na ugonjwa wa kichaa cha mbwa asilimi 96 ni Afrika na asilia huku asilimia 36 ni Afrika, kwa Tanzania kunatakwimu za wanaokwenda hospitali mwaka jana watu walioripoti kung’atwa na mbwa ni 12,680 nchi nzima ,kati yao ni watu sita walifariki", ameongeza Jubilate