Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Kassim auawa na wasiojulikana shambani kwake

Alhamisi , 26th Jan , 2023

Mfanyabiashara mkoani Mwanza Yusuph Kassim, ameuawa na watu wasiojulikana shambani kwake, katika Kijiji cha Chabula wilayani Magu, baada ya kuvamiwa na watu hao akiwa na kijana wake wa kazi ambaye yeye alifanikiwa kuwatoroka watu hao.

Yusuph Kassim, aliyeuawa

Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza Wilbroad Mutafungwa, amesema Jeshi la Polisi mkoani Mwanza limedhamiria kufanya upelelezi wa kina ili kubaini chanzo cha mauaji ya mfanyabiashara huyo.

Kamanda Mutafungwa amesema tarehe 23 ya mwezi huu majira ya usiku mfanyabiashara huyo akiwa shambani kwake na kijana aliyekuwa anamsaidia kazi shambani hapo ghafla wakatokea watu hao na kuwavamia huku kijana huyo akiwatoroka watu hao na kumuacha mfanyabishara huyo hadi kesho yake aliporudi na kuukuta mwili wa mfanyabiashra huyo ukiwa umelala pembeni ya bwawa ukiwa na jeraha kubwa kichwani.

"Marehemu alikuwa anatembelea shamba lake akiwa pamoja na kijana wake wa kazi anayefanya kazi ya kuangalia mifugo, usiku akavamiwa na watu watatu wanaume waliokuwa wameficha sura zao na vitambaa, walimshambulia kichwani kwa kutumia kitu chenye ncha kali, kijana wake alifanikiwa kuwatoroka watu hao na kukimbia ufukweni na kujificha," amesema Kamanda Mutafungwa.

Aidha Kamanda Mutafungwa amesema baada ya kupata taarifa ya tukio hilo polisi kwa kushirikiana na kitengo cha uchunguzi wa sayansi jinai walifika eneo la tukio na kuukagua mwili huo na kuuhifadhi katika hospitali ya wilaya ya Magu huku upelelezi wa tukio hilo ukiendelea hadi watuhumiwa watakapokamatwa.

HABARI ZAIDI

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini