Jumapili , 2nd Aug , 2020

Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) inakaa kikao leo kwa ajili ya kutoa mapendekezo yao kuhusiana na wagombea wa Urais kwa Tanzania Bara na Zanzibar baada ya kufanya utafiti juu ya wagombea hao.

Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe

Akionge na EATV&EARadio Digital msemaji wa Chama hicho Tumaini Makene Leo Agosti 2, 2020 ameeleza kuwa mapendekezo yatakayo tolewa na kikao hicho kwa mujibu wa katiba ya chama hicho yatawasilishwa kwenye kikao cha Baraza Kuu kitakachofanyika kesho Agosti 3, 2020.

"Kamati kuu inakaa kuandaa kwa mujibu wa katiba ya chama kamati kuu inafanya utafiti wa majina ya wagombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar kupitia Kamati Kuu Zanzibar itaanda ajenda kwa ajili ya kupeleka mapendekezo kwenye kikao cha Baraza Kuu".

Kikao hicho cha Kamati Kuu ya CHADEMA kinafanyika katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.