Jumanne , 24th Jun , 2025

Klabu ya Manchester United ipo katika mazungumzo ya mwisho na klabu ya Brentford kwaajili ya kuinasa saini ya mshambuliaji wa timu hiyo Bryan Mbeumo kwa thamani ya Euro millioni 60 ambayo ni zaidi ya bilioni 182 kwa fedha za Tanzania.

Bryan Mbeumo

Zoezi hilo linachagizwa na kocha mkuu wa timu ya Manchester United  Ruben Amorim ambaye ameonyesha nia ya wazi ya kumuhitaji Mcameroon huyo mwenye umri wa miaka 25.

Mbeumo  anashika nafasi ya tatu katika orodha ya vinara wa  uchangiaji wa mabao EPL 2024-2025 ambapo amehusika katika mabao 27 nyuma ya Alexander Isak aliyechangia mabao 29 huku Mohamed Salah akichangia mabao 47 katika

Mbeumo ni mchezaji ambaye United ilimvutia kwa muda na anaonekana kuwa mzuri kwa mfumo wa Ruben Amorim.

Kuna hisia huko Brentford kwamba Mbeumo amepata nafasi ya kuhamia klabu kubwa msimu huu wa joto ikiwa moja itafikia thamani yake.