Alhamisi , 6th Jul , 2017

Rais John Pombe Magufuli ameridhia maombi ya kustaafu mapema kwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Shinyanga Mhe. Prof. John Ruhangisa kuanzia leo Julai 06 mwaka 2017.

Taarifa ya Katibu Mkuu Kiongozi  Balozi John Kijazi amesema kwamba Rais Magufuli ameridhia maombi hayo.

Hata hivyo Jaji Ruhangisa  anaongeza idadi ya majaji walioachia madaraka kabla ya muda wao hivi karibuni.