Msajili wa vyama vya siasa nchini Jaji Francis Mutungi
Jaji Mutungi akizungumza na wawakilishi wa vyama vya siasa kabla ya kuanza kwa zoezi la uhakiki amesema zoezi hilo ambalo mwaka jana lilishindwa kufanyika kutokana na majukumu ya kikosi kazi litafanyika mwaka huu likilenga kukagua hoja muhimu ambazo zilianishwa na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Kuhusu maombi yaliowasilishwa kuhusu usajili Jaji Mutungi amesema maombi hayo ya vyama 18 yatafanyiwa kazi lakini kwanza wakianza kuhakiki vyama vilivyopo kabla ya kupitisha kuendelea na mchakato mwengine.
"Katika hili hatutaki kuona chama kinashindwa kutupa ushirikiano kwa kuwa ni zoezi lenye tija kwa vyama hivyo',' amesema Jaji Mutungi
Nao Profesa Ibrahimu Lipumba Mwenyekiti wa chama cha CUF pamoja na Ana Mlingi Macha Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara wamesema zoezi hilo ni muhimu katika kujenga chama lakini pia ikiwa ni takwa la kisheria .