
Mwandishi wa Habari za Uchunguzi, Erick Kabendera akiwa mahakamani.
ya kukiri makosa yake aliyoiandika ili aweze kusamehewa.
Hayo yamejiri leo Disemba 18, 2019, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, wakati kesi hiyo ilipofikshwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa
Akizungumza mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo Janeth Mtega, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon, amesema kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.
Kabendera anakabiliwa na mashtaka matatu likiwemo la ukwepaji wa Kodi, kuongoza genge la uhalifu pamoja na utakatishaji wa fedha zaidi ya shilingi milioni 170, makosa ambayo anadaiwa kuyatenda kati ya Januari 2015 na Julai 2019, maeneo mbalimbali ya Jiji hilo.