Ijumaa , 16th Mei , 2014

Mishahara duni wanayolipwa askari wa jeshi la polisi nchini Tanzania imeelezwa kuchangia kwa kiasi kikubwa askari kujihusisha na vitendo vya kupokea rushwa.

Mbunge wa Arusha na waziri kivuli wa mambo ya ndani ya nchi, Godbless Lema.

Hayo yameelezwa na Msemaji wa Kambi ya upinzani Bungeni katika Wizara ya mambo ya Ndani mjini Dodoma Mhe. Godbless Lema wakati akitoa hotuba ya Makadirio ya Bajeti Kivuli ya Wizara hiyo.

Naye mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama, Mhe. Lediana Mng'ong'o ameishauri serikali kuongeza bajeti ya chakula kwa mfungwa mmoja kutoka shilingi 500 hadi shilingi 3000 kwa milo mitatu kwa siku.