Chongolo amesema wanashangaa kuona baadhi ya viongozi wakiwemo Mawaziri, wakuu wa mikoa na baadhi ya viongozi wanalalamika kutopewa ushirikiano na watumishi hali ambayo imekishtua chama hicho
Katibu Mkuu Chongolo ametoa onyo hilo mapema leo Jijini Dodoma wakati wakupokelewa kwa Wajumbe wa Sekretarieti mpya ya chama cha Mapinduzi Taifa
Naye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi CCM Sophia Mjema amewataka wasiasa kujibizana kwa hoja na lugha za staha huku akisema wananchi hawataki malumbano bali wanataka kupata Suluhu ya matatizo wanayokutana nayo mitaani