Pongezi hizo zimetolewa na Afisa habari wa BASATA Bwana Artides Kwizela, na kusema kwamba ni suala zuri kukitaka kusukuma ajenda ya kurasimishwa kwa wasanii.
"Napenda kukipongeza kipindi cha Planet Bongo cha East Africa Radio, kwani mbali na kucheza muziki wa wasanii wetu wa nyumbani na kuukuza, lakini kinatoa elimu kwa wasanii kuhusu masuala mbali mbali yahusuyo haki miliki, haki shiriki, lakini vile vile kuwasaidia wasananii kulinda haki zao, big Up East Africa Radio", alisema Kwizela.
Wiki iliyopita Baraza la sanaa la Taifa (BASATA) walipost tweet ikipongeza kipindi hicho, na kusema maneno haya.