Alhamisi , 15th Sep , 2022

Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti amekuwa kocha wa pili kwenye historia ya Ligi ya mabingwa barani Ulaya kushinda michezo 100 ya michuano hiyo, anaungana na kocha wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson ambaye ameshinda michezo 102

Kocha wa Real Madrid Carlo Ancelotti

Ancelotti amefikisha idadi hiyo ya michezo ya ushindi baada ya kukiongoza kikosi cha Real Madrid kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya RB Leipzing mchezo uliochezwa katika Dimba la Santiago Bernabeu.

Mabao ya ushindi ya Madrid katika mchezo huo yamefungwa na Federicio Valverde dakika ya 80 na Marcos Asensio alifunga bao la pili dakika ya 90.