
Kamanda wa Polisi mkoa wa Katavi, Ali Hamad Makame
Kamanda wa polisi mkoani humo Ali Hamad Makame, amesema Jeshi la Polisi likishirikiana na Askari wa hifadhi ikiwa katika doria ya kukamata majangili ilifanikiwa kumnasa.
Akiendelea kutolea ufafanuzi sakata hilo Kamanda Makame, amesema mtuhumiwa bado anaendelea kuhojiwa ili kubaini washirika wake katika kazi hizo za ujangili.