Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana
Hayo ameyasema mkoani Iringa na kuongeza mradi huo unalenga kuongeza idadi ya watalii wanaotembelea hifadhi za Taifa, vivutio vya kiutamaduni na mambo kale nchini na kwamba kupitia wizara na mradi wake wa huo utatekeleza hayo.
“Utekelezaji wa mfumo huu unategemea kwa kiasi kikubwa ushirikiano wetu kama wadau wakuu katika utekelezaji wa mradi wa REGROW, hivyo ninaomba tuutangaze mfumo huu na kuutumia kuwasilisha maoni na malalamiko yatakayotokana na utekelezaji wa mradi,” amesema Balozi Dkt. Chana.