Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Afariki akitaka kuiua familia yake kwa petroli

Jumatatu , 13th Mar , 2023

Hamis Pius (41), mkazi wa Itezi jijini Mbeya, amefariki dunia baada ya kuungua moto alipojifungia ndani ya chumba anacholala na mke wake aitwaye Rebelia Makoso(38) kisha kumwaga mafuta ya petroli na kuwasha moto huku wivu wa mapenzi ukihusishwa na tukio hilo.

Pichani ni miguu ya mtoto iliyoungua wakati akimuokoa mama yake kwenye moto huo

Wakati wa tukio mke wa marehemu alipiga kelele kuomba msaada kwa mtoto wake aitwaye Mkeshilishi Hamis (21), aliyekuwa chumba kingine na alifanikiwa kupiga teke mlango wa chumba na kisha kumuokoa mama yake lakini baba yake alikataa kutoka ndani na kupelekea kuungua hadi kupoteza maisha.

Kwa mujibu wa taarifa ya Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Polisi(ACP) Benjamin Kuzaga, amesema kwamba tukio hilo limetokea Machi 8, 2023 majira ya saa 4:00 usiku.

"Uchunguzi wa awali umebaini kuwa chanzo cha tukio hili ni wivu wa kimapenzi kwa wanandoa hao, lakini  mke na mtoto wa marehemu wanaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali teule ya Ifisi iliyopo Mji mdogo wa Mbalizi wilayani Mbeya, kutokana na majeraha ya moto waliyoyapata mwilini," ameeleza Kamanda Kuzaga.

Hata hivyo Kamanda Kuzaga amelalani tukio hilo na kutoa wito kwa jamii kuachana na vitendo vya kujichukulia sheria mkononi na kuishauri jamii kutatua migogoro yao ya kifamilia na ndoa kwa kukaa meza moja ya usuluhishi badala ya kuchukua maamuzi magumu ikiwemo kutoa uhai.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto