
Moja ya adhabu ambazo hutolewa mashuleni
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. George Simbachawene kupitia hotuba yake iliyosomwa na Mkurugenzi Msaidizi kutoka Ofisi ya Rais katika uzinduzi wa ripoti ya elimu ya msingi nchini amesema, kumekuwa na tabia ya baadhi ya waalimu kutoa adhabu kinyume cha taratibu.
Naye Mratibu wa Mtandao wa Elimu nchini ambao ni wasimamizi wa utafiti huo Bi. Cathrene Sekwao na mtafiti Bw. Jacob Kateri amesema wameamua kufanya utafiti huo ili kuweza kujua hali ya elimu ikoje ili serikali iweze kuona nini kifanyike kuboresha sekta ya elimu ambapo pia wameitaka serikali kupitia mapendekezo yao.