Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Bukoba waomba Soko la kisasa na kituo cha mabasi

Jumatatu , 2nd Jan , 2023

Baadhi ya wakazi wa manispaa ya Bukoba mkoani Kagera wameishauri serikali kutafuta eneo jipya kwa ajili ya ujenzi wa soko kubwa na la kisasa na kukamilisha ujenzi wa kituo kikuu cha mabasi ambacho ujenzi wake umeanza katika eneo la Kyakailabwa, lengo likiwa ni kufungua fursa za kiuchumi

Wakizungumza na EATV wakazi hao wamesema kuwa wanakubaliana na jitihada zinazofanywa na serikali katika kuhakikisha pato la mkoa linapanda, lakini endapo kutajengwa soko kubwa na kituo bora cha mabasi, itachangia uchumi kukua

"Soko letu hili tunalolitumia hivi sasa ni finyu, nashauri lipatikane eneo jingine kwa sababu wafanyabiashara tumekuwa wengi, kipindi kile tunaingia humu miaka kama 25 au 30 iliyopita tulikuwa kama 600 lakini kwa sasa tupo kama 2,000" amesema Ramadhan mfanyabiashara soko kuu

"Bado stand yetu hii inayotegemewa na wenyeji na wageni wanaokuja Kagera ni tatizo hasa mvua zikinyesha panajaa matope, nitafurahi sana endapo stand hii itajengwa maana itakuwa moja ya fursa na kivutio kwa wawekezaji wanaotamani kuja kuwekeza katika mkoa wetu" amesema Mwombeki mkazi wa manispaa ya Bukoba

Akizungumza na waandishi wa habari mkuu wa mkoa wa Kagera Albert Chalamila amesema kuwa katika mwaka huu 2023 kuna fursa nyingi za kiuchumi zitafunguka, na kuwataka wawekezaji kujitokeza kuwekeza katika sekta mbalimbali ikiwamo za kilimo, viwanda na ufugaji

"Fursa mojawapo ni mradi mkubwa ambao una zaidi ya shilingi bilioni 50 kwa ajili ya kujenga stendi ya mabasi, masoko, barabara, kutengeneza taa na kujenga stendi ya malori, utagharamiwa na Rais mwenyewe kupitia World Bank, na fedha hizo Mungu akipenda haitazidi mwezi Machi, nina imani mambo yatakuwa mazuri" amesema Chalamila

Maombi ya wakazi hao ya kukamilishwa kwa kituo kikuu cha mabasi katika eneo la Kyakailabwa yemetolewa wakati mkuu wa mkoa akiwa ametoa kauli hivi karibuni kuwa yanakusanywa maoni ya wadau mbalimbali, ili kuona kama ujezi wa kituo hicho katika eneo hilo uendelee au litafutwe eneo jingine ambalo mabasi mengi yanatokea na hadi sasa majibu ya maoni hayo bado hayajatolewa.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto