Moja ya treni inayomilikiwa na Shirika la Reli kati ya Tanzania na Zambia (TAZARA). Kwa muda sasa usafiri wa mizigo na abiria kati ya Dar es Salaam na Lusaka umekwama kutokana na mgomo wa wafanyakazi wa shirika hilo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na mgeni wake Makamu Mwenyekiti wa Kamisheni kuu ya Ulinzi ya Jeshi la Ukombozi la Watu wa China (PLA) Jenerali Fan Changlong mara baada ya kumaliza mazungumzo yao Ikulu jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Maafisa wa ngazi za juu wa Jeshi la Watu wa China(PLA) pamoja na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)