Timu 72 zinashiriki Esther Bulaya Cup 2014
Timu 72 kutoka katika kata 17 za Jimbo la Bunda Mkoani Mara zimeanza kuchuana hii leo katika Michuano ya Kombe la Easter.
Akiongea na Muhtasari wa Michezo ,Mratibu wa Michuano hiyo ambaye Mbunge wa viti maalum wa Jimbo la Bunda,Ester Bulaya amesema huu ni msimu wa nne wa michuano hiyo huku timu zikiongezeka kutoka 18 mwaka 2011 na kufikia 72 mwaka huu nazo zawadi kwa mshindi ikiongezeka.
Ester Bulaya anesema michuano hiyo imekuwa na hamasa kubwa tangu alipoianzisha huku changamoto kubwa ikiwa ni vifaa kwa timu zinazojitokeza kushiriki michunao hiyo.