Timu 72 zinashiriki Esther Bulaya Cup 2014

Mbunge wa Bunda viti maalum mkoani Mara na Mratibu wa Esther Cup akikagua timu mabingwa wa mwaka 2012,Timu ya Town Star kabla ya mchezo.

Timu 72 kutoka katika kata 17 za Jimbo la Bunda Mkoani Mara zimeanza kuchuana hii leo katika Michuano ya Kombe la Easter.

Akiongea na Muhtasari wa Michezo ,Mratibu wa Michuano hiyo ambaye Mbunge wa viti maalum wa Jimbo la Bunda,Ester Bulaya amesema huu ni msimu wa nne wa michuano hiyo huku timu zikiongezeka kutoka 18 mwaka 2011 na kufikia 72 mwaka huu nazo zawadi kwa mshindi ikiongezeka.

Ester Bulaya anesema michuano hiyo imekuwa na hamasa kubwa tangu alipoianzisha huku changamoto kubwa ikiwa ni vifaa kwa timu zinazojitokeza kushiriki michunao hiyo.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS