Panga la Mwakyembe lawapitia tena watumishi - JNIA

Waziri wa uchukuzi nchini Tanzania Dkt Harrison Mwakyembe.

Serikali ya Tanzania imewasimamisha kazi maafisa 13 wakaguzi katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JK Nyerere kwa tuhuma za kujihusisha na vitendo vya rushwa kwa wageni katika uwanja huo.

Akizungumza leo Jijini Dar-es-Salaam Waziri wa Wizara ya Uchukuzi Dk. Harisson Mwakyembe amewataka maafisa hao kuondoka uwanjani hapo ambapo ametaja wizara wanazotoka kuwa ni Kilimo, Afya na Mifugo.

Dkt. Mwakyembe katika kudhibiti suala hilo kutojirudia ameutaka uongozi wa uwanja huo kuhakikisha kuwa kila afisa anavaa sare pamoja na uwepo ufuatiliaji wa kina wa nyendo zao.

Pages

Subscribe to East Africa Television RSS