TEC yatoa tamko zito kwa Bunge Maalumu la Katiba
Baraza la maaskofu katoliki Tanzania (TEC), limetoa tamko zito kwa wajumbe wa Bunge Maalum la katiba, likiwataka wawe wa moja na kufanya kazi yao kwa mtazamo usioegemea siasa za vyama.
Katika tamko hilo la Mwezi Juni mwaka huu, lililosainiwa na Rais wa TEC, Askofu Tarcisius Ngalalekumtwa na kusoma kwenye ibada za kanisa hilo nchini kote hapo jana, wajumbe hao wanakumbushwa kuwa yeyote anayedharau hitaji la Katiba mpya na anayejaribu kupuuza na kuweka kando rasimu ya pili, huyo si muwakilishi wa watu na kwamba, mwisho wake historia itamuhukumu.

