Mkurugenzi wa kampuni ya Swala Oil and Gas, Abdullah Mwinyi (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na mbunge wa bunge la Afrika Mashariki kutoka Tanzania Bi. Shyrose Bhanji.
Kampuni inayotafiti mafuta na gesi nchini Tanzania ya Swala Oil and Gas, leo imetangaza kuanza kuuza hisa zake ili kila Mtanzania awe sehemu ya umiliki wa rasilimali za mafuta na gesi.