Rais Magufuli awaasa waumini kuiombea Tanzania
Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametembelea Msikiti na Makanisa yaliyopo Chato Mjini Mkoani Geita na kuendelea kuwasihi Watanzania kuombea amani na utulivu katika nchi bila kujali tofauti za dini, makabila na kanda wanazotoka.
