Bakari Malima asema Mshindo Msola hatoshi Yanga.
Nyota wa zamani wa klabu ya soka ya Yanga, Bakari Malima maarufu kwa jina la Jembe Ulaya anahisi kuwa Mwenyekiti wa klabu yao Dr.Mshindo Msola anazidiwa na ukubwa wa timu hiyo au hajapata wasaidizi sahihi ambao wangemsaidia katika kuwaendesha mabingwa hao wa kihistoria wa ligi kuu.

