Che Malone akiri Yanga ni Bora

Beki wa Simba Che Malone Fondo amezungumzia mchezo wa dabi Oktoba 19, 2024 dhidi ya Yanga kwa kusema Wapinzani Wao wanaubora maeneo mengi ndani ya uwanja hivyo kufanya mechi baina yao kutokua rahisi, Che Malone ni mmoja wa Wachezaji wa kutumainiwa kwenye kikosi cha Wekundu wa Msimbazi anafahamu umuhimu wa kushinda mchezo huo kwani wakipoteza watakua wamefungwa kwenye mechi nne mfululizo dhidi ya Yanga
Kuelekea mchezo wa Dabi ya Kariakoo utakaozikutanisha timu za Simba na Yanga beki kisiki wa timu ya Simba amekiri Wapinzani wao ni bora na wana Wachezaji bora kwenye maeno mengi ndani ya uwanja, Che Malone ameyasema hayo siku ya jana Oktoba 8, 2024 kwenye Media Day iliyofanyika Bunju