Wednesday , 26th Jul , 2023

Timu ya Taifa ya wanawake chini umri wa miaka 18 imeanza vyema mashindano ya CECAFA umri wa miaka 18 baada ya kupata ushindi wa goli 3-0 dhidi ya timu ya Burundi katika mchezo wa ufunguzi uliochezwa jumanne Julai 25 , 2023 katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi majira ya saa tisa

Akizungumza na EATV saa moja Kocha Mkuu wa timu hiyo Bakari Shime amesema mechi ilikua nzuri licha ya kwamba wachezaji wake wamecheza  chini ya kiwango  jambo ambalo amelifanyia  kazi na katika mchezo wao kesho julai 27 ,2023 dhidi Ethiopia watakwenda kufanya maajabu.

“Leo tumefanya  mazoezi ya kutafuta utimamu wa mwili kwa wachezaji kuwaelekeza makosa mbalimbali ambayo wamefanya jana na kuwataka wapambane katika kuhakikisha wanafanya vyema katika hatua hii ya makundi”amesema Bakari Shime .

Vile Vile Kocha Shime ametoa maoni ya juu ya  timu za Afrika kuanza vibaya michuano  ya kombe ya dunia ambayo yanafanyika  katika  nchini New Zealand na Australia.

“Ni ndoto ya kila mwalimu siku moja kucheza kombe la dunia hivyo nina mtihani mkubwa wa kuhakikisha siku moja na sisi tunakwenda kushiriki “amesema  Bakari Shime .

Mashindano hayo  yanajumuisha nchi tano kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na Kati ambazo ni Uganda, Ethiopia, Burundi, Zanzibar na Tanzania ambaye ni mwenyeji wa mashindano hayo kwa mwaka huu