
Akiongea na waandishi wa habari Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita Berthaneema Mlay amesema watuhumiwa hao wamefanya tukio hilo baada ya kuambiwa na mganga wa kienyeji kuwa mama yao alimuua mtoto wao
Aidha Mlay ameitaka jamii kuacha kujichukulia sheria mkononi badala yake watoe taarifa kwenye vituo vya Polisi ili watuhumiwa waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria