Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Naibu Waziri Masanja asisitiza mafunzo kwa vitendo

Saturday , 3rd Dec , 2022

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mary Masanja, ameziagiza taasisi za Wizara yake kutenga nafasi za mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) kila mwaka ili kuendana na kasi ya ongezeko la wanafunzi

Ameyasema hayo katika mahafali ya ya 20 ya Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Mwl. Julius Nyerere (JNCC) jijini Dar es Salaam.

Amefafanua kuwa maendeleo ya utalii kitaifa yataweza kufikiwa endapo wadau wote watashiriki katika jitihada za kuelimisha, kuendeleza, kukuza na kuitangaza Tanzania na kwamba kwa kuboresha huduma bora za utalii kutaongeza tija katika sekta hiyo.

“Hatuna budi kuhakikisha kuwa huduma mbalimbali za utalii zinazotolewa zinabeba weledi unaostahili. Weledi huu utaonekana vizuri zaidi katika huduma zetu endapo tutaajiri wataalam wenye ujuzi stahiki kama wanaohitimu leo hii” Mhe. Masanja amesema.

Aidha, ametoa rai kwa wadau wa sekta ya utalii nchini kuhakikisha kuwa huduma mbalimbali za utalii zinazotolewa zinabeba weledi unaostahili na kwamba hilo litaonekana vizuri zaidi kwa vitendo endapo wataajiri wataalam wenye ujuzi stahiki kama wanaohitimu katika chuo hicho.

“Ifike mahali nchi yetu tujivunie kutoa wataalam wanaotosheleza soko la ndani na kupata fursa ya kutoa huduma katika soko la nje kama ilivyo kwa jirani zetu” amesema.

Sambamba na hilo, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanya jitihada za kuhakikisha utalii unaimarika ikiwemo uzinduzi wa Royal Tour ambayo imeleta hamasa kubwa kwa wageni na wenyeji.

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Chuo cha Utalii (NCT), Dkt. Florian Mtey, amewataka wahitimu hao kuzingatia sheria, taratibu, kanuni na miongozo iliyopo ya utumishi wa umma wakatapokuwa wakitimiza majukumu yao wakiwa kazini.
Mahafali hayo yamehudhuriwa na Mabalozi, Wakuu wa Taasisi mbalimbali,Wadau wa Sekta ya Utalii na Ukarimu, Watumishi na Wanachuo,

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP