Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Serikali iangalie watoto wa kike - Lugangira

Tuesday , 26th Jul , 2022

Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Mhe. Neema Lugangira siku ya jana Julai 25, 2022 akiwa katika ofisi za East Africa Television na East Africa Radio alizungumza kuhusiana na kampeni ya Namthamini na juhudi zake katika kuwasaidia wanafunzi wa kike nchini waweze kupata taulo za kike za kujistiri

Mhe. Neema Lugangira akiwa studio za East Africa Radio.

Mhe. Lugangira anasema moja ya vitu ambavyo amejikita navyo kwa mwaka huu ni kuona namna gani ambavyo ataweza kupaza sauti serikali iangalie watoto wa kike mashuleni hususani wa mikoani wanaweza vipi kusaidiwa taulo za kike.

''Watoto wanaotoka katika mazingira magumu hususani watoto wa vijijini mara nyingi wanakosa shule siku 5 mpaka 7 kila mwezi kwa sababu tu ya kuwa kwenye hedhi, na wanakosa shule kwa sababu hawana nyenzo sahihi za kujistiri kwa maana ya taulo za kike, na pale ambapo wanakwenda shule wanatumia vitu ambavyo ni hatarishi kwa mfano mabanzi, magazeti, nyasi na vitu ambavyo vinaweza kuwapelekea kuwaweka hatarini kupata kansa'' alisema Mhe. Neema Lugangira.

#

Pia Mhe. Lugangira amesema katika kipindi cha bunge la bajeti 2022/23 lililomalizika hivi karibuni, aliweza kuishauri serikali katika mradi wa maendeleo wa TASAF waone namna ambavyo wataweza kuwasaidia watoto wa kike wanaotoka katika kaya maskini waweze kupata taulo za kike.

Aidha, Mhe. Lugangira ameipongeza East Africa Television na East Africa Radio kwa juhudi zao katika kuwasaidia wanafunzi mashuleni kupitia kampeni ya Namthamini ambayo hufanyika kila mwaka tangu mwaka 2017.

Mhe. Lugangira amepaza sauti mara nyingi bungeni kuhusiana na mtoto wa kike, na mwaka jana kupitia kampeni hii alichangia taulo za kike kwa wanafunzi 42 kwa mwaka mzima.

HABARI ZAIDI

Bujukano Mahungu John, Mwenyekiti wa Umoja wa Waganga na Wakunga wa Tiba Asili Tanzania

Waganga wa jadi waungana kukemea ukatili, Geita

Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Mvua zilizoambatana na upepo zimeua watu watano TZ

Muonekano wa Eneo la Somanga baada ya Mawasiliano kati ya Lindi na Dar es Salaam kurejeshwa.

Mawasiliano yarejeshwa barabara ya Dar - Lindi

Naibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga

Kituo cha kupoza umeme kujengwa Tunduma

Mkuu wa Usalama Barabarani mkoa wa Songwe Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Bukombe, akizungumza na abiria

"Fungeni mikanda muda wapo safarini" - SSP