Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mbatia kuondolewa kwenye orodha ya Viongozi NCCR

Thursday , 26th May , 2022

Msajili Msaidizi wa vyama vya siasa Tanzania Sisty Nyahoza amesema kuwa baada ya kumuandikia barua James Mbatia na kumjulisha kusimamishwa kuwa Mwenyekiti wa Chama hicho hatua inayofuata sasa ni kuondoa jina lake kama moja ya viongozi wa Chama

Kiongozi huyo amesema nafasi yake itakaimisha kwa Makamu Mwenyekiti Zanzibar .

Nyahoza akizungumza na earadio amesisitiza kuwa utaratibu wa kumuondoa kiongozi huyo ulifuata taratibu zote na uamuzi ulikuwa halali

"Sisi baada ya kuwaandikia barua NCCR - Mageuzi kinachofuata sasa ni kusajili mabadiliko ya Uongozi, ndio Sheria inavyosema, kwahiyo sasa hivi tunaweka pembeni jina la Mbatia na nafasi yake anakaimu yule Makamu Mwenyekiti Zanzibar" 

Kuhusu tuhuma alizotoa James Mbatia jana kuwa Ofisi ya Msajili imeshiriki kufadhili mkutano uliomuondoa madarakani, kiongozi huyo amekana tuhuma hizo na kusisitiza ofisi ya msajili haihusiki na hilo 

"Sio kazi ya Ofisi ya msajili wa vyama vya siasa kugharamia mikutano ya vyama, sisi tulialikwa tu,  mbona tulialikwa vya CHADEMA hawasemi tulifadhili, NCCR - Mageuzi wana matatizo yao ndani ya chama wasituletee sisi, kama wana shida zao sisi kazi yetu ni kuangalia nani yupo kwa mujibu wa sheria" amesema Nyahoza

"Sisi tumesema ule mkutano ulikuwa sahihi na Mbatia ameondolewa kihalali, ndio jambo la msingi akae pembeni, mtu ukiona kabisa wenzako hawakutaki ndani ya Chama shida yako nini?, anaongea na vyombo vya habari badala ya kuja Ofisi ya Msajili, tunamkaribisha sana hata leo aje"

"Vyama vya siasa viheshimu Sheria na Katiba zao, vina migogoro mingi kwa sababu wanabishana sana kugombea madaraka, wanakuwa na tamaa ya mali, kama NCCR - Mageuzi walikuwa na masuala ya migogoro ya mali za chama, mambo yameanza siku nyingi na sio sisi tuliyapeleka huko ni wao wenyewe walianzana huko" 

"Sisi baada ya kuwaandikia barua NCCR - Mageuzi kinachofuata sasa ni kusajili mabadiliko ya Uongozi, ndio Sheria inavyosema, kwahiyo sasa hivi tunaweka pembeni jina la Mbatia na nafasi yake anakaimu yule Makamu Mwenyekiti Zanzibar" ameeleza Sisty Nyahoza , Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu