Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Rais Samia akutana na wafanyabiashara wa Ufaransa

Monday , 16th May , 2022

Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewakaribisha Rasmi Tanzania, Ujumbe wa Shirikisho la Wafanyabiashara wa Sekta Binafsi kutoka nchini Ufaransa MEDEF pamoja na Taasisi ya Biashara ya Ufaransa Business France, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2022.

Akizungumza na Wajumbe hao ambao kati yao ni Makampuni 41 pamoja na Wajumbe 50, Rais Samia amesema huo ni mwanzo mzuri kwa makampuni hayo kuja kuangalia fursa mbalimbali za kibiashara pamoja na uwekezaji zinazopatikana nchini.

Rais Samia amesema kwamba Makampuni hayo yamekuja kutokana na Ziara yake ya Kikazi aliyoifanya nchini Ufaransa ambapo pamoja na mambo mengine alikutana na kuzungumza na Rais wa nchi hio Emmanuel Macron pamoja na kushuhudia utiaji Saini wa Mikataba mbalimbali ya kibiashara kati ya Tanzania na Ufaransa.

Katika Kikao chake na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, Mhe. Rais Samia amesema walikubaliana mambo kadhaa ikiwepo kuendeleza ushirikiano wa siku nyingi baina ya nchi hizi mbili.

Rais Samia amebainisha kuwa Tanzania ni Sehemu ya salama ya Uwekezaji na atahakikisha anaondoa vikwazo vyote katika uwekezaji na ufanyaji wa biashara nchini.

Mhe. Rais Samia amewakaribisha Wajumbe hao kuitembelea Bandari ya Dar es Salaam ili kujionea ufanisi wake, vivutio mbalimbali vya Utalii kama Mlima mrefu kuliko yote Barani Afrika Mlima Kilimanjaro, Mbuga ya Wanyama Serengeti pamoja na Kisiwa cha Zanzibar kwasababu wamepata fursa ya kuja nchini.  

Kwa upande wa Makamu Mwenyekiti ambaye ni Kiongozi wa Ujumbe huo wa Wafanyabiashara kutoka Ufaransa Bw. Gerard Wolf amesema kuwa Wameitikia wito alioutoa Mhe. Rais Samia kwa wao kuhakikisha wanakuja nchini Tanzania mapema mara baada ya ziara yake ya Kikazi nchini Ufaransa. 

Bw. Wolf amesema kuwa katika Ujumbe waliokuja nao nchini, yapo Makampuni 41, na Wajumbe 50 kwa ajili ya kuja kuangalia fursa mbalimbali za Uwekezaji na kufanya Biashara nchini Tanzania.

Bw. Wolf amesema wamekuja Tanzania ajili ya Biashara na tayari makampuni pamoja na Wafanyabiashara kutoka Ufaransa yanafanya vizuri na wanategemea kwenda mbali zaidi katika Uwekezaji wao hasa 
sekta ya Nishati jadidifu, Tehama, sekta mbalimbali za kiuchumi. 

Amebanisha kuwa hata katika kipindi cha janga la ugonjwa wa Uviko 19, makampuni na wafanyabiashara wa Ufaransa hawakuondoka nchini ili kuhakikisha wanatimiza malengo yao ya kufanya kazi kwa bidi kwa kujali muda na Mafanikio ya pande zote.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani