Friday , 22nd Apr , 2022

Mkurugenzi wa Elimu ya Mlipa Kodi kutoka TRA, Richard Kayombo, amesema kwamba lengo la kukutana na wataalam wa kampuni ya Meta inayomiliki Facebook, Instagram na WhatsApp, ni kuchukua hatua ambazo huko mbeleni watakavyoweza kuchangia kodi nchini.

Mkurugenzi wa Elimu ya Mlipa Kodi kutoka TRA

Kauli hiyo ameitoa hii leo Aprili 22, 2022, kwenye kipindi cha Supa Breakfast cha East Africa Radio, na kusema kwamba mkutano wa awali walioketi hapo jana na wataalam hao ulikuwa ni wa wao kuelewa mazingira ya sheria ya kodi pamoja na wao kueleza jinsi wanavyotozwa kodi kwenye nchi zingine.

"Lengo ni kufikia mahali huko mebeleni kampuni hiyo iweze kuchangia kodi kutokana na biashara inayofanyika hapa nchini kupitia mitandao yao, wananchi wasiwe na hofu," amesema Richard Kayombo