Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Griezmann aokoa Jahazi la Ufaransa, Euro 2020

Saturday , 19th Jun , 2021

Timu ya taifa ya Ufaransa imebanwa mbavu na Hungary kwenye mchezo wa Kundi F’ kwenye muendelezo wa michuano ya Euro 2020, baada ya timu hizo kutoka sare ya bao 1-1.

Antoine Griezmann

Kwenye mchezo ambao mabingwa wa Dunia Ufaransa walipewa nafasi kubwa ya kuibuka na ushindi lakini walijikuta wanakibarua cha kutafuuta bao la kusawazisha baada ya Hungary kupata bao dakika ya 45 kupitia kwa mchezaji Attila Fiola. Lakini baadae kipindi cha pili kunako dakika ya 66 Antoine Griezmann akaifungia bao Ufaransa na kuufanya mchezo huo kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Sasa mabingwa hao wa Dunia wanafikisha alama 4 na ndio vinara wa kundi F’ wakati Hungary wapo nafasi ya 3 wakiwa na alama 1 walioipata leo.

Mchezo unaofata wa kundi F’ tutawashuhudia mabingwa mara tatu wa ulaya timu ya taifa ya Ujerumani wakiutafuta ushindi wa kwanza baada ya mchezo wa raundi ya kwanza kufungwa na Ufaransa kwa bao 1-0, hivyo wanahitaji ushindi au sare ili kufufua matumaini ya kusonga mbele kwenye michuano hii, na wanakibarua kigumu mbele ya mabingwa watetezi Ureno ambao wao mchezo wa kwanza walishinda mabao 3-0 dhidi ya Hungary na ushindi kwa ureno utawahakikishia nafasi ya kusonga mbele hatua ya 16 bora. Mchezo huu utapigwa majara ya Saa 1:00 Usiku.

Na mchezo wa mwisho leo utachezwa Saa 4:00 Usiku ambao ni mchezo Pekee wa kundi E’ Hispania wataumana na timu ya taifa ya Poland. Hispania ina alama moja baada ya kutoka sare ya bila kufungana kwenye mchezo wa kwanza dhidi ya Sweeden, wakati Poland ilipoteza kwa kufungwa na Slovakia pkwa mabao 2-1.

Hispania ambao pia ni mabingwa mara tatu wa ulaya wapo kwenye presha kubwa kufuatia kiwango kilichoonyeshwa na safu yao ya ushambuliaji kwenye mchezo wa kwanza tofauti na matokeo ya ushindi hii leo itawaweka katika mazingira magumu ya kutinga hatua ya 16 bora.

HABARI ZAIDI

Mkuu wa mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko,

Wadau wa afya simamieni ukusanyaji mapato

Picha za Kuonesha Muelekeo wa Kimbunga IALY

Kimbunga IALY charipotiwa bahari ya Hindi

Mabaki ya Nyumba yenye vyumba 12 iliyoteketea na Moto

Moto wateketeza nyumba yenye vyumba 12

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya