Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

ACT wataja sababu za kumchagua Othman Masoud

Tuesday , 2nd Mar , 2021

Katibu Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, amesema kuwa waliamua kumpendekeza Othman Masoud, awe mrithi wa Maalim Seif, kwa sababu ya misimamo yake na uwezo wake uliojipambanua kuhusu maslahi ya Zanzibar na ni mtu ambaye hakutaka sifa za kisiasa.

Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Othman Masoud

Kauli hiyo ameitoa hii leo Machi 2, 2021, kwenye kipindi cha Supa Breakfast cha East Africa Radio, na kuongeza kuwa mchakato wa kupendekeza jina haukuwa rahisi kwani walihitaji mtu ambaye angeweza kuvaa viatu vya Maalim Seif, na kwamba kati ya wanasiasa wote wa Zanzibar hakuna ambaye ameweza kumtilia shaka Othman Masoud.

"Othman Masoud ukiwachambua wanasiasa wa Zanzibar hakuna hata mmoja ambaye atamtilia mashaka katika misimamo yake juu ya maslahi ya Zanzibar na yeye ameshawahi kuonesha misimamo mikubwa isiyotarajiwa pale maslahi ya Zanzibar yanapotishiwa na wakati akiwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar alichukua msimamo wa kuipinga Katiba inayopendekezwa katika vifungu visivyozingatia maslahi ya Zanzibar," ameeleza Ado Shaibu.

Jana Februari Mosi, 2021, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Mwinyi, alimteua Othman Masoud, kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar na ameapishwa hii leo.

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani