Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wafungwa 1789 wa ethiopia wapata msamaha wa JPM

Monday , 25th Jan , 2021

Rais Sahle -Work Zewde leo amewasili nchini Tanzania kwa ziara ya siku moja na kukutana na mwenyeji wake Rais John Magufuli wilayani Chato mkoani Geita.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Ethiopia Mhe. Sahle-Work Zewde mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Geita leo, Januari 25, 2021 kwa ziara ya kikazi ya siku moja.

Akizungumza katika hafla ya ukaribisho,Mh. Rais John Magufuli amesema nchi ya Ethiopia imepiga hatua katika sekta ya mifugo ikiwa ni nchi ya kwanza barani Afrika kwa kuwa na mifugo mingi, huku Tanzania ikiwa ya pili kwa mifugo na bado hatua haijapigwa katika sekta hii.

''Waethiopia wanatengeneza  mabegi, mikanda, viatu na kuuza nje ya nchi yao na bidhaa zao zina soko kubwa barani Ulaya, hivyo nimemuomba Mh. Rais Sahle, tupate wawekezaji  pia na sisi tuende kujifunza kutoka kwao'' amesema Rais Magufuli.

Aidha  Rais Magufuli amesema kwa upande mwingine mazungumzo yao yalilenga katika kuwaachia wafungwa 1789 wa Ethiopia ambao waliingia nchini kinyume cha sheria na kuhukumiwa kwa mujibu wa sheria za nchi, namna ya kupanga mbinu za kuwarudisha nyumbani kwao bila masharti yoyote, maana sisi ni ndugu.

Pia tumezungumza kuhusu ushirikiano zaidi hasa katika masuala ya kiuchumi, pia tumemuomba mh. Rais ashughulikie tupate eneo la kujenga ubalozi nchini Ethiopia na wao nimewakaribisha Dodoma wajenge ubalozi wao.

Kwa upande wake Rais wa Ethiopia Mh.Sahle -Work Zewde amesema amefurahi kutembelea nchini Tanzania na hasa katika eneo ambalo ni chanzo cha mto Nile katika ziwa Victoria, ambapo maji yake wanayatumia  hivyo ameahidi kuongeza ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

''Tunahitaji ushirikiano imara katika nchi hizi mbili, katika maeneo ya biashara na uwekezaji tukiamini ni lazima Afrika tuwekeze hivyo eneo la mifugo ni eneo la kipaumbele '' amesema Rais Sahle

Pia Rais Sahle amemshukuru Rais Magufuli kwa kuwaachia wafungwa waliokuwa wahamiaji haramu wote 1789 wa Ethiopia, na kuaahidi kuwarudisha nyumbani mara moja na kuondoa mzigo kwa Tanzania.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu