Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Magufuli awashukuru waumini wa dini ya kiislamu

Friday , 27th Nov , 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli, amewashukuru viongozi na waumini wa dini ya kiislamu pamoja na wa dini nyingine nchini kwa kuliombea Taifa katika kipindi cha miaka mitano ya awamu ya kwanza ya Serikali ya Awamu ya Tano na amewasihi waendelee na utaratibu huo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli.

Kauli hiyo imetolewa leo Ijumaa, Novemba 27, 2020, na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, baada ya kuswali swala ya Ijumaa katika msikiti wa Msalato jijini Dodoma.

"Wakati najiandaa kuja kuswali nilimuaga Mheshimiwa Rais na ameniagiza nilete salamu zenu kwamba anawashukuru sana kwa kumuunga mkono, amesema kuwa mbali na viongozi hao na waumini kumuunga mkono katika awamu ya kwanza ya uongozi wake, pia walitoa ushirikiano mkubwa katika kipindi cha kampeni kwa kuendelea kuliombea Taifa hadi uchaguzi ukafanyika kwa amani",amesema Waziri Mkuu kwa niaba ya Rais Magufuli.

Waziri Mkuu amesema kuwa, Rais Dkt. Magufuli, amewaomba viongozi hao wa dini pamoja na waumini waendelee kuliombea Taifa na viongozi wake ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa amani na utulivu.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu amewasisitiza viongozi hao waendelee kuwahamasisha waumini washiriki ibada mbalimbali kwa sababu, jambo hilo ni muhimu na linapaswa kufanyika kwa kuzingatia muda, pamoja na kuwasihi waumini hao kuwazoesha watoto wao kufanya ibada ili wawe watoto wema.

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu