Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Al Ahly na Zamalek ni vita ya kisasi fainali CAFCL

Friday , 27th Nov , 2020

Miamba ya soka Afrika vilabu vya Al Ahly na Zamalek vyote vya nchini misri vinataraji kukutana kwenye mchezo wa fainali ya michuano ya klabu bingwa Afrika mchezo unaotazamiwa kupigwa leo kwenye dimba la Cairo International nchini misri saa 4 kamili usiku kwa saa za Afrika ya mashariki.

Picha za mashabiki wa timu zote mbili

Mchezo huo unatazamiwa kuwa wakisasi kutokana na uhasimu wa kihistoria wa wawili hao kwenye ligi kuu misri na ubabe wa Al Ahly mbele ya Zamalek wa kuwafungwa kwenye michezo 5 na sare 3 Zamalek akiwa hajamfunga mpinzani wake huyo wa jadi kwenye michuano hiyo mikubwa Afrika.

Kocha wa klabu ya Ahly Pitso Mosimane aliyejiunga na klabu hiyo mwezi septemba anapewa nafasi kubwa ya kutwaa taji hilo baada ya kuwahi kuwafunga Zamalek 3-1 mwaka 2016 na kutwaa kombe hilo akiifundisha Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini kabla ya kujiunga na Al Ahly.

Mosimane akifanikiwa kutwaa taji hilo basi atakuwa kocha watatu kwenye historia kuwahi kutwaa mataji hayo mara mbili akitwaa moja na klabu tofauti baada ya kulitwaa taji hilo mwaka 2016 mbele ya Zamalek.

Kwa Upande wa kocha wa Zamalek Mreno Jaime Pacheco amesema ana imani na ubora walionao wachezaji wake na kudai unaweza kuwafurahisha mashabiki zake kwa kufanya vizuri.

Mchezo huo unataraji kuingia kwenye vitabu vya historia kwa kuwa mchezo wa kwanza wa fainali ya michuano hiyo kuchezwa na vilabu viwili kutoka taifa moja, kuchezwa bila mashabiki na kuchezwa mchezo mmoja tokea mabadiliko ya kuacha kucheza michezo miwili ya fainali.

Mashabiki hawataruhusiwa kuingia uwanjani kuutazama mchezo huo kutokana na katazo lililotolewa na mamlaka ya afya na shirikisho la soka nchini misri kuchukua tahadhari ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa hatari wa korona unaoendelea kusumbua nchini misri na maeneo mengine dunia.

Ugonjwa wa Korona umeviathiri vilabu vya Al Ahlay na Zamalek ambao baadhi ya wachezaji na kocha msaidizi wamepatwa na ugonjwa wa korona siku chache zilizopita. Walid Soliman, Mahmoud 'Kahraba' Abdelmoneim na Saleh Gomaa ni wachezaji wa Al Ahly wenye COVI-19.

Kwa upande wa Zamalek, Mahmoud 'El Wensh' Hamdy na kocha wake msaidizi Medhat Abdelhady wameambukizwa maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19.

Mshindi wa kombe hilo anataraji kuweka kibindoni dola za kimarekani milioni moja sawa na bilioni mbili na milioni 319 za kitanzania wakati makamu bingwa akitaraji kupokea dola za kimarekani laki saba na nusu sawa na shilingi bilioni moja milioni mia saba thelathini na tisa.

Ikumbukwe kuwa, Al Ahly ndiye klabu bingwa kihistoria kwa kutwaa kombe hilo mara 8 wakati Zamalek wakibeba mara 5.
 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani