Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Je, historia imewabeba mawaziri wa JPM?

Friday , 30th Oct , 2020

Katika awamu yake ya kwanza Rais John Magufuli, aliunda Baraza lake la kwanza la Mawaziri tarehe 10 Desemba 2015 ambalo alilitangaza kwa awamu mbili huku likiwa na mawaziri 19 katika wizara 18 ambapo katika orodha hiyo hakuwa amezijaza nafasi nne za uwaziri ambazo alizijaza wiki mbili,

Pichani ni Wabunge wateule, kushoto ni Mh. Jenista Mhagama (Peramiho), Mh. Ummy Mwalimu (Tanga Mjini), kulia ni Mh Dkt Philip Mpango (Buhigwe).

baadaye tarehe 23 Desemba.

Katika awamu yake ya kwanza ya kipindi chote cha miaka mitano Rais Magufuli alifanya mageuzi kadhaa yakiwemo mageuzi makubwa kwa madogo katika nafasi za uwaziri ikiwemo kuwaondosha kabisa mawaziri kwenye baraza au kuwahamisha na kuwabadilisha wizara huku wengine wakiwa hawajaguswa kwa kipinde chote cha miaka mitano zaidi wakisifiwa kwa utendaji wao.

Mawaziri hao sita ambao waliweza kuepukana na wimbi la tumbua tumbua pia walijitokeza katika kinyang'anyiro cha kuwania nafasi za ubunge katika maeneo yao, kando na Dkt. Hussein Mwinyi aliyejitosa kuwania Urais huko Visiwani Zanzibar na kuibuka na ushindi wa kura 380,402.

                                          Rais Mteule wa Serikali ya Mpinduzi Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi

Mawaziri hao ni pamoja na Dkt. Philip Mpango (Wizara ya Fedha na Mipango), Prof Joyce Ndalichako, (Elimu), Wiliam Lukuvi (Ardhi na Maendeleo ya Makazi), Jenista Mhagama (Sera, Bunge,Vijana) na Ummy Mwalimu (Afya).

Pichani ni Wabunge Wateule, Kushoto ni Mh.William Lukuvi (Isimani), kulia ni Mh Prof Joyce Ndalichako (Kasulu Mjini)

Aidha wabunge hawa ambao utendaji wao katika wizara zao ulitajwa kuwa wa mfano pia kumpendeza Rais, tayari wametangazwa kushinda katika majimbo yao ambapo Mpango amepata kura (Buhigwe 43,481), Ndalichako (Kasulu Mjini 49,390), Lukuvi (24,934), Mhagama (Peramiho, 27,479), Ummy (Tanga Mjini114,445).

 

HABARI ZAIDI

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa